Babalevo Azungumzia Tetesi za Rayvanny Kuondoka WCB

[Picha: Rayvanny Instagram]

Mwandishi: Brian Sikulu

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Msanii maarufu kutoka Tanzania Babalevo ametoa kauli yake kuhusu tetesi za Rayvanny kuondoka lebo ya WCB. Tetesi hizo zimetamba mtandaoni haswaa baada ya Rayvanny kuanzisha lebo yake ya Next Level Music.

Maswali pia yameibuka kuhusu lebo ya WCB kutotambua mafanikio ya Rayvanny kimuziki kama vile hapo zamani.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Rayvanny Aachia Video Mpya Ya ‘Rara’

Babalevo ambaye pia ni mtangazaji wa Wasafi FM, na pia amejulikana kama msemaji wa lebo ya WCB, katika mahojiano ya hivi karibuni aliulizwa iwapo Rayvanny ameondoka lebo ya WCB.

Kwa mujibu wa Babalevo, Rayvanny kuondoka WCB sio jambo mbaya, bora iwe kwa amani na makubaliano.

Alieleza kuwa hakuna haja ya msanii kuwa katika lebo wakati anahisi amekua zaidi. Aliongeza kuwa iwapo Rayvanny hajajipanga kuwa msanii huru basi ni vyema asalie katika lebo ya WCB ili aendelee kupata manufaa ya lebo hiyo.

Soma Pia:  Nyimbo Mpya: The Ben Aachia ‘Why’ Akimshirikisha Diamond Platinumz [Video]

"Mimi sioni kama ni kitu kibaya, kama Rayvanny ameona amefikia hatua ametosheka utaratibu upo nadhani watakuwa wamemuwekea yeye. Akitoka kwa amani na upendo sioni kama kuna ubaya wowote," Babalevo alisema.

Licha ya tetesi hizo kusheheni mtandaoni, Rayvanny bado anafanya kazi na lebo ya WCB kwa ushirikiano na lebo yake ya Next Level Music.

Katika kazi yake mpya ya 'Rara' kwa mfano, mtayarishaji wa muziki aliyehusika katika kuusuka mdundo huo ni Ayo Lizer kutoka WCB.

Leave your comment