Collabo 10 Kali Kutoka Tanzania Zilizofanya Vizuri Zaidi Mwaka 2021

[Picha: Beka]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

kufanya kazi na wasanii wengine aidha kutoka ndani au nje ya Tanzania ili kutengeneza kazi nzuri. Zifuatazo ni collabo kumi kali ambazo zimeachiwa na wasanii kutokea nchini Tanzania kwa mwaka huu:

Soma Pia: Wasanii 10 Bora Tanzania Kwa Mwaka 2021

Baikoko - Mbosso ft Diamond Platnumz

Hii ni moja kati ya collabo zilizotesa sana kwa mwaka 2021 na hii ni kutokana na ushirikiano mzuri ulioonekana baina ya Mbosso na Diamond Platnumz.

https://www.youtube.com/watch?v=hGqzvvbZnyQ

Ndombolo - Ali Kiba ft Abdu Kiba & Tommy Flavour

Hii ni ngoma ambayo inaonesha wazi ufundi na uwezo mkubwa walionao Kings Music kwenye suala zima la utunzi na uandishi wa muziki. Colabo hii iliwaleta pamoja wasanii wote walio chini ya Kings Music.

https://www.youtube.com/watch?v=Cf-5DuXPMzY

Ex Wangu Remix - Seneta Kilaka ft Hamisa Mobeto

‘Ex Wangu Remix’ ni moja kati ya ngoma za singeli ambazo zimepamba sana mwaka 2021. Hii imechagizwa na wazo zima la wimbo kuwa la kibunifu pamoja na ushirikiano mzuri  wa kisanaa uliooneshwa kati ya Seneta Kilaka na Hamisa Mobetto.

https://www.youtube.com/watch?v=CmSgffQYaSo

Beer Tamu - Marioo ft Tyler ICU, Visca & Abbah Process

Huenda ikawa ndio ngoma ya Amapiano iliyotamba zaidi Bongo kwa mwaka 2021. Hii ni kutokana na namna ambavyo Marioo ameimba vizuri kwenye ngoma hii akitumia mdundo wenye nguvu ambao umetayarishwa na Abbah Process na Tyler Icu.

 https://www.youtube.com/watch?v=J5Ka53RZUtE

Kushki - Chege ft Saraphina

Ushirikiano mzuri kati ya Chege na Saraphina kwenye ‘Kushki’ umepelekea ngoma hii kuwa na uraibu wa kupitiliza hasa kwenye sehemu ya kiitikio ambacho mwanamuziki Chege ameweza kukitendea haki.

https://www.youtube.com/watch?v=TttpK5SjXb8

Lala - Rayvanny ft Jux

Wimbo huu uliweza kumkutanisha Rayvanny ambaye husifika kwa uwezo mkubwa wa kuimba pamoja na Jux ambaye wengi humsifu kwa sauti yake ambayo hutaradadi sana kwenye muziki wa RnB.

https://www.youtube.com/watch?v=s3kdjHUPlXA

Unaua Vibe - Rapcha ft Young Lunya & Dwin

Moja kati ya collabo bora zaidi ya Hiphop kwa mwaka 2021. Hii ni kutokana na shauku ya mashabiki kuwa na hamu ya kumsikia Rapcha na Lunya kwenye ngoma moja. Baada ya ngoma hii kufanya vizuri hapa Tanzania, miezi minne baadae Rapcha aliachia ‘Unaua Vibe Remix’ akiwashirikisha Femi One na King Kaka kutokea Kenya.

https://www.youtube.com/watch?v=Ul5c6i0SL80

For Your Love - Mbosso ft Zuchu

Hii ni ngoma ambayo imezidi kuthibitisha uwezo wa Mbosso kwenye uandishi wa nyimbo na uwezo alionao Zuchu kwenye kuimba pindi anaposhirikiana na Mbosso. Kupitia mitandao ya kijamii kama Tikitok, Instagram na Snapchat mashabiki wengi hasa wa kike wameonekana kuvutiwa sana na ngoma hii.

https://www.youtube.com/watch?v=3GHmlVDSRPA

Iyo - Diamond Platnumz ft Focalistic, Mapara A Jazz & Ntosh Gazi

Kupitia collabo HII, Diamond Platnumz amezidi kudhihirisha anaweza kufanya kazi na msanii anayeimba aina yoyote ya muziki hapa barani Afrika.

https://www.youtube.com/watch?v=UcOSSs3CNQ0

Jealous - Ali Kiba ft Mayorkun

Kutoka kwenye albamu yake ya ‘Only One King’, ngoma ya Jealous haikufanya vizuri tu nchini Tanzania bali kila upande wa Afrika hasa ukitegemea kuwa ilikuwa ni moja kati ya ngoma chache ambazo Alikiba alishirikiana msanii kutokea nje ya Afrika Mashariki.

https://www.youtube.com/watch?v=LQyCY1t--GU

Leave your comment