Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nandy Afunguka Kutupilia Mbali Tamasha Kadhaa Juu ya Malipo Duni
20 May 2021

[Picha: Nandy Instagram]
Mwandishi: Branice Nafula
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Msanii tajika wa Bongo fleva Nandy amesema kuwa yeye na usimamizi wake wamelazimika kuacha tamasha nyingi kutokana na malipo yasiyo ya thamani yao.
Soma Pia: Zuchu vs Nandy: Ni nani Bora Zaidi?
Akizungumza katika hafla ya kuzindua ushirikiano wa tamasha lake la Nandy Festival, mwimbaji huyo amesema kuwa matarajio yake katika shows ni kupata hela zaidi ya milioni nane.
"Me na management yangu tumeshaacha shows kibao zile ambazo tunaona hazitupi thamani yetu, tumeshaacha show kibao za millions 8 au 7 kutokana na hatuioni thamani yetu, na show inapokuja vibaya upande wetu huwa tunaamini tu sio riziki yetu," alisema Nandy .
Soma Pia: Wasifu wa Nandy, Nyimbo Zake Bora, Tuzo Alizoshinda, Mahusiano na Thamani Yake
Kupitia tamasha la Nandy festival, Nandy amepanga kupeleka burudani kwa wakazi wa Kigoma, na miji zingine za Tanzania kasha avuke Kenya ambapo anapanga kuwa na show Nairobi na Mombasa.
Vile vile, Nandy alisema kuwa mipango ya miaka ijayo ni kupeleka tamasha hili hadi nchi zingine na wa sasa wapo wenye mazungumzo upande wa Burundi. Wasanii pia watakua wengi tofauti na miaka iliyopita.
"Mwaka huu Nandy Festival itafanyika kwenye mikoa 7 Tanzania, tutaenda pia Nairobi na Mombasa kwa upande wa Kenya lakini bado tupo kwenye mazungumzo kwa upande wa Burundi! Mwaka huu tutakuwa na list ya Wasanii wasiopungua 12 na surprises kibao humo ndani,” alisema Nandy.
Weekly Top 10 songs

KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
CHAMPION GAL3:00
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- NEW SONG ALERT
16 May
- Generation
16 May
- Boom Shakatah means
17 May
- Date of birth
15 May


Leave your comment