Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA – Nikiachana na muziki nahamia kwenye siasa – Diamond
25 January 2016

Diamond Platnumz amesema akiachana na muziki anataka kuwa Waziri wa Habari, Tamaduni na Michezo ili kuweka vitu sawa na kutoa fursa zaidi kwa vijana.
Akizungumza katika kipindi cha Papaso cha TBC FM, Diamond alisema kama akiingia kwenye siasa basi nia yake ni kuwa Waziri wa Michezo.
“Kwa hivi sasa bado ila nikiingia kwenye siasa baadaye, akimaliza mheshimiwa Nape nachukua mimi kile cheo cha Waziri wa Michezo”.
“Kile nakiweza kabisa kwasababu mimi ukiniambia sijui kuhusu mpira, movie mimi naweza kabisa nikiwa waziri, nikavifanya na vikawa na mendeleo. Ni kitu ambacho naweza siyo nasema nataka kuwa mbunge ila mimi nataka ile siku nimeacha kufanya muziki naingia kwenye siasa basi nakuwa Waziri wa Habari, Tamaduni na Michezo na kuboresha vitu”, aliongeza Diamond.
Diamond ambaye hakusema kwamba ataingia kwenye siasa kupitia chama gani, mwaka jana katika kampeni za uchaguzi mkuu
uliomuingiza Rais Mgufuli madarakani, alishiriki kikamilifu kwenye kampeni za CCM na kutengeneza wimbo pamoja na video.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- new update don cast
25 May


Leave your comment