Nyimbo Mpya: Micky Singer Na Maua Sama “Moyo Wangu”


[Picha: Instagram]

Mwandishi-Charles Maganga 

DOWNLOAD LATEST BONGO MUSIC MP3

Mwanamuziki nguli kutoka Tanzania, Micky Singer amerudi tena kwenye kiwanda cha muziki Tanzania na ngoma yake mpya ya kuitwa “Moyo Wangu” akiwa na Maua Sama. 

Moyo Wangu ni ngoma ya tatu kutoka kwa Micky Singer kwa mwaka huu baada ya hapo awali kuachia “Jishaue” akiwa na Tommy Flavour pamoja na “Nobody” aliyoitoa mwezi mapema mwaka huu. 

Pakua Mixes Ndefu Zaidi Ndani Ya Mdundo

Moyo Wangu ni wimbo mzuri mapenzi ambapo ndani yake Micky na Maua Sama wanarushiana mashahiri mazuri ambayo bila shaka yatakuburudisha. Ngoma hii imetayarishwa na mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania wa kuitwa Elipoano. 

Huu ni ujio mpya wa Micky Singer ambaye mapema mwaka huu alitajwa kuwania Tuzo Ya Msanii Bora Kiume Chipukizi kwenye Tuzo za  Tanzania Music Awards 2023. 

Leave your comment