Amepotea: Mbosso Kivingine Na Ngoma Mpya


[Picha: Instagram]

Mwandishi-Charles Maganga 

Nyimbo Mpya Tanzania Wiki Hii

Baada ya ukimya wa takriban miezi mitano tangu aachie EP yake ya kuitwa “Khan” msanii Mbosso kutokea WCB amerudi tena na ngoma mpya kabisa ya kuitwa “Amepotea”

Ikumbukwe kuwa Mbosso wiki chache zilizopita, alishinda tuzo moja katika Tanzania Music Awards kama Msanii Bora Wa Bongo Fleva kwenye tuzo hizo. 


Kwenye ngoma yake hii mpya ya kuitwa “Amepotea”, Mbosso anachukua nafasi ya mwanaume anayetafutwa kwa hali na mali na familia yake baada ya yeye kutoroka na kuhamia kwa mpenzi wake ambako anapewa mahaba mazito. 

“Amepotea” imetayarishwa na S2kizzy ambaye ni mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania ambaye ameshafanya kazi na wasanii wakubwa mbalimbali huku video ikiwa imetayarishwa na Director Ivan.

 

Leave your comment