Nyimbo Mpya: Rich Mavoko 'Blow Up', Fid Q 'Kiberiti' na Ngoma Zingine Zilizoachiwa Bongo Wiki Hii

[Picha: Kenyan Digest]

Mwandishi: Charles Maganga

Pakua Ngoma za Maua Sama Bila Malipo Kwenye Mdundo

Mashabiki wa muziki kutoka Tanzania wameendelea kupokea burudani kali kutoka wasanii ambao ndani ya wiki hii wametoa nyimbo mpya, ambazo zimezidi kunawirisha na kukuza kiwanda cha muziki nchini Tanzania. Zifuatazo ni ngoma tano mpya kutoka nchini Tanzania kwa wiki hii: 

Bad Man - Tunda Man ft Harmonize 

Hii ni moja kati ya collabo bora kabisa ambayo kwa sasa imezidi kutikisa nchini Tanzania. Kinachovutia zaidi kwenye "Bad Man" ni video yake ambayo imefanyika kwa ubunifu mkubwa na kwa kutumia ustadi wa hali ya juu.

https://www.youtube.com/watch?v=RS9PMaKJHQ4

Soma Pia: Tundaman ft Harmonize 'Badman', Jay Melody ft Marioo 'Sugar' Remix na Nyimbo Zingine Zinazovuma Bongo Wiki Hii

Lala - Mimi Mars ft Marioo 

Ukiweka kando tetesi za mahusiano  zinazoendelea kati ya Mimi Mars na Marioo, kitu kingine kinachofanya wasanii hawa waongelewe sana ni nyimbo hii mpya ya kuitwa 'La La'. Video ya ngoma hii imeongozwa na Director Kenny na kufikia sasa imeshatazamwa mara laki mbili arobaini na tatu kwenye mtandao wa YouTube. 

https://www.youtube.com/watch?v=S4mcZTt2EY4

Kiberiti - Fid Q ft Saida Karoli

Kiberiti ya Fid Q bila shaka imewasha moto kiwanda cha muziki Tanzania wiki hii kutokana na nyimbo hii kubeba ujumbe mzito na mafunzo kadhaa.  Kitu kingine kinachpondeza ni mwanamuziki wa nyimbo za asili Saida Karoli kupamba ngoma hii na sauti yake ya kuvutia kwenye kiitikio. 

https://www.youtube.com/watch?v=BkcZ6Le5i7c

Nikuone Remix - Dayoo ft Kusah 

Ufundi na umakini wa Dayoo kwenye muziki wa Bongo Fleva umezidi kuonekana baada ya kinda huyo kumshirikisha Kusah kwenye ngoma yake ya kuitwa 'Nikuone Remix'. Ndani ya ngoma hiyo, Dayoo anatoa sifa nyingi kwa mpenzi wake ambaye anamtaja kuwa ni mzuri kisura na kitabia. 

https://www.youtube.com/watch?v=eQZWbDTFh_w

Blow Up - Rich Mavoko Fid Q 

Huu ni wimbo makhususi kabisa kwa wale wote wanaopenda kujivinjari na kula raha kwenye sehemu mbalimbali za starehe. Kupitia mashairi ya ngoma hii, Rich Mavoko anamshawishi mpenzi wake waende kula raha katika maeneo tofauti tofauti huku Fid Q nae akitumia vyema talanta yake ya kurap kusindikiza ujumbe huo.

https://www.youtube.com/watch?v=xRfSI7fdlhY

Leave your comment