Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya: Zuchu Aachia 'Mwambieni’
21 January 2022

[Picha: Free Music]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mwanamuziki mashuhuri kutokea Tanzania Zuchu ameachia ngoma yake mpya kabisa ya kuitwa ‘Mwambieni’.
‘Mwambieni’ ni ngoma yenye vionjo vya Afro-Pop na ndani yake Zuchu anatuma ujumbe kwa mpenzi wake wa zamani kuwa aache kumfuatilia na kumuuliziia mara kwa mara kwani yeye ameshaendelea na maisha yake.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Nandy Aachia Video ya ‘Party’ Akiwashirikisha Billnass na Mr Eazi
‘Kaja omba nirudia kazirejesha salamu zamani kakumbukia ameumisi utamu kaacha kopa kalamba garasa kaishiwa masikini. Mpeni taarifa za beti mkwasa mi simkumbuki sini," anaimba Zuchu kwenye aya ya kwanza.
‘Mwambieni’ inakuja takriban mwezi mmoja tangu Zuchu aachie ngoma yake ya ‘Kitu’ huku ngoma hii pia ikiwa ni ngoma ya kwanza kwa mwaka 2021.
Ngoma hii inatarajiwa kufanya vizuri kutokana na mashahiri yake kuwa rahisi kukaririka na kuimbika. Kabla ya ngoma hii kutoka, Zuchu kwa muda mrefu sasa amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kuwajuza watu kuwa atatoa ngoma hivi karibuni.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Tommy Flavour Aachia Ngoma Mbili Mpya ‘Lay Down’ na ‘Kidogo’
Ngoma hii imetayarishwa na Mr Lg mtayarishaji wa muziki ambaye kando na kazi hii, pia ameshafanya kazi na Zuchu kwenye ‘Litawachoma’ ngoma ambayo Zuchu alifanya na Diamond Platnumz na kuweza kufanya vizuri sana.
Kufikia sasa, bado ‘Mwambieni’ haina video ila huenda malkia huyo kutoka WCB akaachia video ya ngoma hio hivi karibuni.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April


Leave your comment