Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya: Rich Mavoko Aachia Video ya ‘Sio Leo’
13 January 2022

[Picha: Rich Mavoko Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Baada ya subira ya takriban mwezi mmoja sasa, hatimaye Rich Mavoko ameachia video ya ngoma yake pendwa kabisa ya kuitwa ‘Sio Leo’ ambayo amemshirikisha Big Zulu kutokea Afrika Kusini.
Ngoma ya ‘Sio Leo’ iliingia sokoni mwezi Desemba mwaka 2021 na hii ni ngoma ambayo ndani yake Rich Mavoko anamshukuru Mungu kwa matendo yake makuu aliyomtendea na hasa kwa kumtoa kwenye hali duni na kumpatia maisha mema.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Rayvanny Aachia Video ya 'Stay' Akimshirikisha Abby Chams
Ukisikiliza kwa umakini ngoma hii ni dhahiri shahiri kuwa maudhui na ujumbe uliomo unatukumbusha ngoma ya 2019 Ommy Dimpoz ya kuitwa ‘Ni Wewe’ pamoja na ngoma ya Tommy Flavour ya mwaka 2020 ya kuitwa ‘Jah Jah’ ambayo amemshirikisha Ali Kiba.
Video ya ‘Sio Leo’ imefanyika huko nchini Afrika Kusini na hii ni video ambayo imesheheni stori nzuri ambayo bila shaka imerandana vizuri na mashahiri yaliyomo kwenye ngoma hii ambayo Rich Mavoko anaonekana akiimba kwa hisia sana.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Killy Aachia Video ya 'Ni Wewe' Akimshirikisha Harmonize
Aidha, ubora wa picha ambao ni wa viwango vya juu pamoja na mandhari yaliyotumika kwenye video hii ya ‘Sio Leo’ yameifanya kanda hii ambayo ni ya kwanza kwa Rich Mavoko kwa mwaka 2022 kuwa yenye viwango vya juu.
Kufikia sasa, video ya ngoma hii imeshatazamwa mara kumi na tano elfu kwenye mtandao wa YouTube.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- MOSS Kay
24 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- Naphlic_fx
24 April


Leave your comment