Nyimbo Tano Zilizofanya Vizuri TikTok Kwa Mwaka 2021

[Picha: YouTube]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Ukweli ni kwamba TikTok ni mojawapo kati ya mitandao ya kijamii ambayo ina watumiaji wengi sana hapa nchini Tanzania na mara nyingi watumiaji wa mtandao huu hutumia nyimbo za wasanii mbalimbali pindi wanapojirekodi video. Zifuatazo ni ngoma tano kali kutoka Tanzania ambazo zimefanya vizuri zaidi Tiktok kwa mwaka 2021.

Soma Pia: Bifu Tano Kubwa Kwenye Bongo Fleva Mwaka 2021

Naanzaje - Diamond Platnumz

Huenda ikawa ndio ngoma iliyofanya vizuri zaidi kwa Afrika Mashariki kwenye upande wa Tiktok. Kufikia sasa, hashtag ya wimbo huu kwenye Tiktok imeshatazamwa mara Milioni 45 kwenye mtandao huo. Hii imechagizwa hasa na mashahiri mazuri yaliyopamba ngoma hii.

https://www.youtube.com/watch?v=iKbW2EDs_mE

Sukari - Zuchu

Mashahiri yake mepesi ambayo watu wengi wa jinsia ya kike walikuwa wanaweza kuyaimba kwa urahisi ni kitu ambacho kimefanya ‘Sukari’ kuwa ni wimbo bora sana kwa watumiaji wa Tiktok kwa mwaka 2021. ‘Sukari Challenge’ ambayo ni hashtag iliyoanzishwa na Zuchu kufikia sasa imeshatazamwa mara Milioni 22.5 kwenye mtandao wa Tiktok

https://www.youtube.com/watch?v=CCmItvVgn6Q

Soma Pia: Nyimbo Tano Kutoka Tanzania Zilizozua Utata Mwaka wa 2021

Kubali - Lody Music

Tangu ulipoachiwa Septemba 4 mwaka huu, ‘Kubali’ ya Lody Music ni ngoma ambayo ilipokelewa kwa mikono miwili na watumiaji wa Tiktok. Hii ni kutokana na ujumbe na mashahiri ya ngoma hii kuwa ya kugusa moyo hasa kwa, wale watu ambao wameumizwa na mapenzi.

https://www.youtube.com/watch?v=isMW61ztn5Y

Huba Hulu - Jay Melody

Mdundo mkali kutoka kwa Genius Jini pamoja na uandishi mzuri kutoka kwa Jay Melody ilipelekea mashabiki wengi hasa kutokea Tanzania na, Kenya kuupenda wimbo huo na kwenye mtandao wa Tiktok. Kufikia sasa, hashtag ya Huba Hulu kwenye mtandao huo imeshatazamwa mara Milioni 5.5.

https://www.youtube.com/watch?v=GC0Qao0YUW8

Beer Tamu - Marioo

Huitaji kuwa na mahaba na pombe ili uweze kurahani ngoma hii ambayo kutokana na mdundo wake kuwa wa kuvutia watu wengi wanaotumia Tiktok walipenda kutumia ngoma hii kwenye video zao.

https://www.youtube.com/watch?v=J5Ka53RZUtE

Leave your comment