Mshindi wa Mdundo.com DJ Battle Kutuzwa Shilingi Milioni 7 za Tz

2021 Mdundo.com DJ Battle inatazamiwa kuanza nchini Tanzania siku ya Ijumaa, tarehe 19 Novemba, 2021. Shindano hilo litakalodumu kwa wiki 4, litamshuhudia DJ mmoja akitawazwa ‘King of The Turntable.’

Mshindi atakabidhiwa mkataba wa udhamini wenye thamani ya Tsh 7,000,000. Mixtape ya atakeyeshinda itapata kuchezwa kwenye redio na pia kwenye hafla kubwa ya muziki.

Ni Nani Anayestahiki?

Shindano liko wazi kwa DJs wote. Aina yoyote ya muziki inaweza kuingia kwenye shindano, iwe ni Afropop, Hausa, Amapiano, Hiphop, Gospel...e.t.c

Jinsi ya Kutuma Maombi?

Tembelea mdundodjbattle.com ili kujiandikisha na kuanza kupakia mchanganyiko.

Leave your comment