Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Rapcha Azungumza Baada ya Profesa Jay Kumfananisha na Mangwair
18 October 2021

[Picha: The Citizen]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Rapa kutokea nchini Tanzania Rapcha amefunguka ya moyoni baada ya rapa Profesa Jay kufananisha aina yake ya muziki na ile ya marehemu Albert Mangwair.
Kupitia akaunti yake ya Instagram siku mbili zilizopita, Professa Jay alimpongeza Rapcha kwa muziki mzuri anaoufanya na kumfananisha na marehemu Albert Mangwair.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Mac Voice Aachia Video Mpya 'Pombe' Akiwashirikisha Rayvanny na Leon Lee
"Huyu Dogo ananikumbusha uwezo mkubwa sana wa marehemu Albert Mangwair wa kipaji kikubwa cha kuweza kuimba na kuchana kwa mpigo. Namuona mbali sana," aliandika Profesa Jay.
Akiongea na kituo cha Times FM, Rapcha amemshukuru sana na Profesa Jay kwa kuamini kipaji chake kiasi cha kumfananisha na Mangwair na ameahidi kufanya kazi nzuri zaidi.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Cheed Aachia Ngoma Mpya ‘Final’
"Hii ni call ya kunikumbusha kwamba mimi ni nani na nina kitu gani ndani yangu na nnahitaji kukipeleka wapi. Enough respect kwa yeye kuweza kutake time yake. Mi naapreciate sana hicho kitu," alizungumza Rapcha.
Uwezo wa Rapcha kwenye muziki wa Rap unaonekana zaidi kwenye albamu yake ya ‘Wanangu 99’ ambayo imesheheni ngoma 10. Ukisikiliza ngoma ‘Nitakucheki’ au ‘Kama Unae’, uwezo wa Rapcha unaonekana vilivyo. Rapcha yuko chini ya lebo ya mtayarishaji wa muziki nguli kutokea Tanzania P Funk Majani ambaye ana wasifu wa kufanya ngoma na wasanii wakubwa Bongo kama Mangwair, Professa Jay, Fid Q na wengineo wengi.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April
- Nordman--Kelly yo collabo
30 April
- One and only
01 May


Leave your comment