Sina Chuki na Diamond- AT Aeleza ya Kufanya Kazi na Konde Worldwide

[Picha: Citi Muzik]

Mwandishi: Brian Sikulu

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Mwanamuziki wa Tanzania AT amefunguka kuhusu historia ya urafiki wake na Diamond Platnumz. Hii inakuja siku chache baada ya AT kukosolewa na baadhi ya mashabiki wake kwa kufanya kazi na Anjella kutoka Konde Worldwide Music.

Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walidai kuwa haikuwa sahihi AT kufanya kazi na Harmonize. Walielezea kuwa ushirikiano wake unaweza kumaanisha kwamba sasa alikuwa mpinzani wa Diamond Platnumz.

Soma Pia: AT Azungumzia Uhasama wa Jadi Baina ya Diamond na Alikiba

Akizungumza wakati wa mahojiano ya hivi karibuni, AT alifafanua kuwa hana chuki yoyote dhidi ya bosi wa WCB. Aliendelea kuelezea zaidi kuhusu historia ya urafiki wake na Diamond.

Kulingana na AT, alikuwa mmoja wa wanamuziki wachache waliomuunga mkono Diamond Platnumz wakati bado alikuwa mchanga kwenye muziki. Alifunua kuwa Diamond na mkewe walikaa nyumbani kwake kwani hawakuwa na pesa za kutosha kukodisha nyumba.

Muimbaji huyo ambaye hivi karibuni aliachia wimbo uliopewa jina "Si Saizi Yako", alidai kwamba alishiriki pakubwa katika mafanikio ya Diamond kwenye tasnia ya muziki.

Soma Pia: Anjella Amshirikisha AT "Si Saizi Yako’: Nyimbo Mpya Tanzania [Official Audio]

AT alibainisha kuwa anamwona Diamond kama kaka na bado anaendelea hadi sasa, akiongeza kuwa kamwe hawezi kumchukia Diamond.

"Mimi sikuwahi kuwa na chuki na Nasibu… Watu wengi hawalijui hili, wimbo wa Mbagala, Diamond asingeuupata kwa muda ambao alikuwa anatarajia," AT alisema.

Leave your comment