Kutoka Kuitwa Sayuni Choir Getak Kisha Sayuni Singers Tz hadi "Sayuni Choir Tz"

Moja kati ya kwaya inayovuma sana Kupitia wimbo "Bwana Yesu awaita" ilifanya mabadiliko ya jina lake katika baadhi ya akaunti zake za mitandao ya kijamii. Mwanzo ilijulikana kama "sayuni choir getak" ikaamua kubadili jina na kuitwa "sayuni singers tz" mnamo tarehe 24 mwezi huu na tarehe 25 ilibadilisha jina lake kwenye account ya mdundo, youtube na instagram kuwa Sayuni Choir Tz, na mnamo tar 14 tiktok pia tumebadilisha jina kuwa Sayuni Choir Tz huku facebook ikitumia "sayuni dnpc getak" lakini username/handle name ikiwa ni "sayunichoirtz" kwa tiktok, facebook na youtube, kwa instagram ni "sayunichoir.tz"
Kwa mujibu wa manager anayesimamia akaunti zake anasema kuanzia sasa watatumia jina la "Sayuni Choir Tz" na wataziandika akaunti zao zote(ikiwemo facebook ) kwa kutumia jina hilo. Wote wanaotufuatilia watatupata kupitia jina hilo. "kwa sasa tumeanza na tiktok, youtube na instagram lakini baadaye tutamalizia na facebook" alisema.

Leave your comment