Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Dayna Nyange Aeleza Kwanini Anataka Kupenya Soko la Muziki Nchini Nigeria
11 June 2021

[Picha: Dyana Nyange Instagram]
Mwandishi: Brian Sikulu
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mwanamuziki wa Tanzania Dayna Nyange ambaye anakua kwa kasi katika tasnia ya muziki ameibuka kuelezea kwanini analenga kupenya kwenye tasnia ya muziki ya Nigeria.
Dayna Nyange aliachia kollabo yake ya kwanza na Davido katika wimbo uliopewa jina la 'Ello' ambao ulipokelewa vizuri kati ya mashabiki wake.
Soma Pia: Dayna Nyange Afunguka Jinsi Alivyomshawishi Davido Kufanya Collabo Naye
Dayna katika mahojiano ya hivi karibuni ambayo alifanya alipofika Tanzania kutoka Nigeria, alifunua kwamba alikuwa ametumia muda mrefu kusoma muziki wa Nigeria. Aliongeza kuwa alikuwa amekaa karibu mwezi mzima nchini Nigeria kabla ya kusafiri kurudi Tanzania.
Dayna Nyange alielezea kuwa ni ngumu kwa mwanamuziki yeyote kufanikiwa Nigeria haswa kutoka Afrika Mashariki. Hata hivyo, alikuwa amejitolea kufanikiwa Afrika Magharibi kwa sababu tasnia yao ya muziki ndio iliyoendelea zaidi barani Afrika.
Soma Pia: Zuchu Nyimbo Mpya: Ngoma Tano Zilizomfanya Zuchu Kuwa Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki
Dayna alifichua kuwa wanamuziki wa Nigeria wana kipato kizuri kutokana na muziki wao, na kuongeza kuwa ni rahisi msanii kujiorodhesha kati ya watakaoongoza Afrika iwapo atashinda tasnia ya muziki ya Nigeria.
Dayna alikuwa mwanamuziki wa pili wa Kitanzania baada ya Diamond kutoa collabo na Davido.
"Tasnia ya muziki ya Nigeria imebanana sana. Sio rahisi kupenya. Yaani ukiona sisi watu ambao tunaowafahamu ukiwataja wasanii wa Nigeria, unaweza taja ata watano sita na wote wawe wanafanya vizuri.
"Lakini ukienda Nigeria ni tofauti sana, kwa hivyo mimi ni mtu ambaye nimekua nikienda kule na kurudi na nikasoma soko la kule," Dayna alisema.
Weekly Top 10 songs

KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
CHAMPION GAL3:00
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- NEW SONG ALERT
16 May
- Generation
16 May
- Boom Shakatah means
17 May
- Date of birth
15 May


Leave your comment