TANZANIA: Christian Bella atumbuiza Ikulu jana

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Jumanne hii alimwandalia dhifa ya Taifa, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Joseph Kabila Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Joseph Kabila wakiagana na viongozi wastaafu Ikulu jijini Dar es salaam

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkali wa masauti Christian Bella alikuwa mmoja kati ya wasanii ambao walialikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya kusherehesha shughuli hiyo. Angalia picha.

 

Mama Janeth Magufuli akimtuza mwanamuziki Christian Bella kwa kutumbuiza wimbo maarufu wa “Nani kama Mama” kwenye dhifa hiyo

 

Msanii mkongwe Zahir Ally Zorro alikuwepo kutoa burudani

 

Spika Mstaafu Mhe Anne makinda akimtuza mwanamuziki Christian Bella kwa kutumbuiza wimbo maarufu wa “Nani kama Mama” kwenye dhifa hiyo

 

Mama Salma Kikwete akimtuza mwanamuziki Christian Bella kwa kutumbuiza wimbo maarufu wa “Nani kama Mama” kwenye dhifa hiyo

 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akimtuza mwanamuziki Christian Bella kwa kutumbuiza wimbo maarufu wa “Nani kama Mama” kwenye dhifa hiyo

 

 

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

Leave your comment