Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: "Tusimdharau Chidi Benz" – Fid Q
16 March 2016

Rapa mahiri nchini Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q amefungukia suala la rapa anayefananishwa nae kimichano maarufu kama Stamina kukanusha kujiita Chid Beenz.

Stamina
Akizungumzia suala hilo katika mahojiano yake na kipindi cha Planet Bongo ya East Afrika Radio rapa huyo amesema hashangai watu kumfananisha na Stamina kimashairi na kuongeza kuwa kila mtu anatambua kuwa Stamina amewahi kutangaza kufuata nyayo zake na amekuwa akifanya hivyo kwenye nyimbo zake.

Chid Benz
Akizungumzia suala la Chid Beenz rapa huyo ameeleza kuwa bado anaamini uwezo wa Chid Beenz hivyo hakuna sababu ya kumdharau kutokana na kupotea kwake kwenye game, huku akieleza kwa jinsi anavyo amini uwezo wa Chid Beenz hakuna kinacho mshinda kwenye staili ya michano.
Chanzo: Mtembezi.com
Weekly Top 10 songs
Top stories
- OXEN MUSIC
29 July
- Mytee boy - SURVIVE
28 July
- Abakuchinsali
29 July




Leave your comment