TANZANIA: O’G imenifungulia milango ya kimataifa – G Nako

<p style="text-align: justify;"><img src="/media/articles/1454672357_5094_b.jpg" alt="" /></p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">Rapa anayeunda kundi la Weusi, G Nako amesema wimbo wake mpya wa &lsquo;OG&rsquo; unaofanya vizuri kimataifa, umemfungulia milango kwa kuanza kupokea simu za kufanya kolabo na wasanii toka nje ya Tanzania.</p>
<p style="text-align: justify;">Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha East Afrika Radio Alhamis hii, G Nako alisema kazi hiyo huwenda ikampa deal kubwa za kimataifa.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Kazi imetoka nje na kuna baadhi ya simu zinakuja wanataka kolabo na vitu kama hivyo. Kwahiyo inavyozidi kupasua anga, ndivyo ninavyoendelea kujiandaa kwa kazi mpya&rdquo;.</p>
<p style="text-align: justify;">Pia G Nako aliongeza, &ldquo;Kuna vitu vingine vingi ambavyo vinakuja. Lakini cha kushukuru wimbo umetoka nje na watu wameuelewa na wao ndio wanaotaka kufanya kolabo na sisi. Hiyo inatuonyesha kwamba kitu chetu ambacho tunakifanya kipo katika level kubwa ambayo imewafanya wasanii wa nje watutafute kwa ajili ya kolabo&rdquo;.</p>

Leave your comment