TANZANIA: Tunda amtaka Matonya kumpa maksi za uandishi ya wimbo wa Vailet!

<p style="text-align: justify;"><img src="/media/articles/1454586257_0891_b.jpg" alt="" /></p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">Msanii wa muziki toka kundi la TipTop Connection, Tunda Man amemtaka msanii mwenzake Matonya akubali kuwa yeye ndiye aliyemwandikia wimbo wa Vaileth ili tofauti zao za muda mrefu zimalizike.</p>
<p style="text-align: justify;">Waimbaji hao ambao mwaka 2015 walipatanishwa na kituo kimoja cha radio na kudai wataingia studio kuandaa wimbo wa pamoja, lakini hadi sasa bado wanaendelea kutupiana maneno.</p>
<p style="text-align: justify;">Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio Jumatano hii, Tunda alisema kuwa Matonya anatakiwa akubali ili mambo yaishe.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Kila kitu ye anakijua, ndio maana mi nasema yeye ndo ana-create hivi vitu vinatokea ugomvi, yeye ndo anataka viwepo, anajua kila kitu kuhusu Vaileti, anachotakiwa kufanya ni kuwaambia tu wananchi kuwa alichosema kuwa Tunda alifanya hii ngoma, aliandika mimi nimeimba lakini ilitakiwa nay eye aimbe lakini alishindwa kwahiyo nikaimba mimi ngoma yote&rdquo;, alisema Tunda Man.</p>

Leave your comment