TANZANIA – Hiki ndicho kilichompoteza Saida Karoli – Mrisho Mpoto

<p style="text-align: justify;"><img src="/media/articles/1453730513_0559_b.jpg" alt="" /></p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">Mrisho Mpoto amesema moja ya sababu zilizofanya kupotea kwa msanii wa nyimbo za asili, Saida Karoli ni kukosa uongozi mzuri wa kusimamia kazi zake mwenyewe.</p>
<p style="text-align: justify;">Akizungumza kupitia kipindi cha Sunrise cha Times FM Ijumaa iliyopita, Mpoto alidai kuwa msanii huyo hakuwa na usimamizi mzuri japo alikuwa na uwezo mkubwa kwenye Sanaa.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Ilifika kipindi kila kitu akawa anafanya yeye mwenyewe, hakuwa na uongozi mzuri sana, lakini naamini akisimamiwa hata sasa atarudi vizuri tu&rdquo;, alisema Mjomba.</p>
<p style="text-align: justify;">Kwa upande mwingine Mpoto amewataka Watanzania kuzikumbatia tamaduni zao na kuachana na umagharibi, kwani kufanya hivyo ni sawa na kupigwa &lsquo;pingu&rsquo; za akili.</p>
<p style="text-align: justify;">Wakati huo huo ambapo Mpoto ameachia wimbo mpya uitwao &lsquo;Sizonje&rsquo; hivi karibuni amewataka mashabiki wake kumpigia kura kwenye tuzo za Kora 2016.</p>

Leave your comment