EXCLUSIVE (TANZANIA) – Album ya Cinderella iliuza copy milioni 2 –Ali Kiba

 

 

Staa wa muziki Tanzania King Kiba anayetamba na kibao cha ‘Chekecha Cheketua’ asema kuwa album yake ya kwanza ya Cinderella iliuza nakala milioni 2 (double platinum).

Akizungumza katika kipindi cha XXL cha Clouds FM alisema hajawahi kusikia rekodi hiyo kama imewahi kuvunjwa na msanii mwingine yoyote Tanzania.

“Kiukweli album yangu ya kwanza ya Cinderella ndiyo ilivunja rekodi na sijasikia mpaka leo rekodi hiyo imevunjwa” , alisema. “Sijui (nakala) ni milioni mbili vile, kitu kama hicho, kila album ilikuwa inauzwa mia mbili”, alisema Kiba.

Japo aliingiza zaidi ya milioni 200 King Kiba alisema utoto ulikuwa mwingi.

“Nilijenga kupitia album, vitu vingi  nilifanya, yaani mpunga nilikuwa ninao alafu nilikua sijua kama ninao.Wewe unafikiri nilipumzika bure” aliongezea mwanamuziki huyo.

Leave your comment