EXCLUSIVE (TANZANIA)- Sharobaro Records kuleta mapinduzi (Bob Junior)

 

 

Msanii na mtayarishaji wa muziki, Bob Junior,  amesema anakuja kuleta mapinduzi kwa ujio wa kazi za wasanii wanaotokea kwenye label yake ya “Sharobaro Records” katika muziki. Bob Junior amesema kuwa tayar ana wasanii kama 5 na anaamini watakuja kuleta changamoto katika muziki wa Bongo Fleva.

“Sharobaro Records kuna kazi nyingi zinakuja, hasa hasa tuna wasanii 5 wanakuja rasmi”, alisema Bob Junior, aliongeza “Hawa ni wapya na wanakuja na ladha mpya ili kuleta ladha mpya.Sharobaro tunatambua umuhimu wa kukuza vipaji kwahiyo wadau wasubirie kazi. Mimi na timu yangu tutasikiliza ngoma za wasanii wote na kupanga ipi ichukuliwe na itoke. Nitachukua ngoma mbili kutoka kwa kila msanii na kukaa na wadau wangu na kuchuja ipi safi” aliongeza.

Source: Bongo5

Leave your comment