"Hits Only" Diamond Athibitisha Collabo Yake Na Darassa Iko Mbioni

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Baada ya tetesi za muda mrefu hatimaye, msanii Darassa amedokeza kuwa yuko mbioni kuachia collabo na msanii kutokea lebo ya WCB, Diamond Platnumz. 

Darassa ambaye aliupamba mwaka 2023 na hits zake mbili ambazo ni Nobody akiwa na Bien pamoja na I Don't Care amedokeza ujio wa collabo hiyo ambayo mashabiki wamekuwa wakiisubiri kwa muda mrefu. 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Darassa alichapisha video ambayo inamuonesha akiwa na Diamond Platnumz na kuandika:

“WCB Big Boss Diamond Platnumz ametoa go ahead sasa mabibi na mabwana boys and girls tukutane hapa 22nd” 

Diamond alijibu chapisho kwa kuandika “HITS ONLY” kauli iliyothibitisha kuwa huenda wawili hao wanaachia mkwaju wao wa pamoja tarehe 22 mwezi February. 

 

 

 

 

 

Leave your comment