NEVER REVIEW BY BRUCE AFRICA 

 

Kupitia ngoma zake kama You, Slow pamoja na Jojina ni dhahiri kuwa Bruce Africa ni moja ya wasanii wa kutegemewa sana kwenye kiwanda cha muziki wa Tanzania kwa sasa. 

Download Bruce Music For Free on Mdundo

Ngoma yake ya kufungulia mwaka 2024 ya kuitwa Never ni kithibitisho kingine tosha kuwa kinda huyu ambaye amepata malezi ya kimuziki kutoka kwa wasanii kama Christian Bella na Country Wizzy, ni mwanamuziki haswa. 

 

Kwenye Never, Bruce Africa amechanganya muziki wa aina mbili yaani Kazomba pamoja na Bongo Flava na kwenye ngoma hii, Bruce anatumia sauti yake kumsifia mpenzi wake. 

 

Bila shaka kwa wapenzi wa muziki kutoka Tanzania, Never ni ngoma ambayo itaenda kuwa kivutio kwenye masikio na hii kutokana na jitihada kubwa alizozionesha mtayarishaji wa ngoma hii, Producer Wambaga ambaye pia ana wasifu wa kufanya kazi na wasanii wengine kutoka Tanzania kama Country Wizzy pamoja na Harmonize. 

 

Video ya Never imeshatoka na  imetayarishwa na Director Travellah ambaye ni gwiji kwenye uandaaji wa video za muziki kutoka Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujuml

Leave your comment