Ngoma Mpya : Gnako Atangaza Kufanya Kaz Na Wasanii Bongo


Picha: Facebook
mwandishi:Charles Maganga

Rapa kutoka Bongo G Nako, ambaye kwa sasa anatamba na wimbo “Shuga Daddy” ambao ameshrikiana na Juma Jux, hivi karibuni ametangaza kwamba yuko mbioni kuachia ngoma mpya ambayo ameshirikisha wasanii watatu wakubwa kutoka Tanzania

Rapa huyo ambaye pia ni mshiriki kwenye kundi la Weusi ameweka wazi kwamba hivi karibuni ataachia collabo akiwa ameshirikisha wasanii wakubwa. G Nako ni rapa maarufu Tanzania ambaye ametamba na ngoma kama “Gusanisha” “Original” na nyinginezo nyingi 

Akiwa kwenye mahojiano hivi karibuni, G Nako amedokeza kwamba tayari ana ngoma ambayo ndani yake amemshrikisha Whozu, Juma Jux na Jay Melody 

“Kuna (ngoma) nyingine inakuja. Yuko Whozu, kuna Jay Melody, niko mimi alafu yuko Jux”  alizungumza G Nako kwenye mahojiano na XXL. 

G Nako sio mgeni kwenye uwanja mzima wa collabo. Kufikia sasa rapa huyo ameshashirikiana na wasanii wengine wengine kutoka Tanzania ikiwemo Vanessa Mdee, Shetta, Ben Pol, Maua Sama na wengineo wengi. 

Leave your comment