Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Rick Ross Adokeza Kufanya Remix Na Navy Kenzo
8 May 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi-Charles Maganga
DOWNLOAD LATEST BONGO MUSIC MP3
Tasnia ya muziki nchini Tanzania imeendelea kunawiri na hii ni baada ya hivi karibuni msanii kutokea huko nchini Marekani, Rick Ross kuomba collabo kwa kundi la muziki Tanzania, Navy Kenzo.
Rick Ross ameomba collabo hiyo kutoka kwa Navy Kenzo hivi karibuni kwenye mtandao wa Instagram pindi Navy Kenzo na Rick Ross walipokuwa Insta Live.
Rick Ross ambaye jina lake halisi ni William Leonard Roberts III akiwa anazungumza na Navy Kenzo hivi karibuni amesema kuwa yuko tayari na angependa kushiriki kwenye remix ya “Sip N Whine” ambao ni wimbo namba 6 kwenye album ya Navy Kenzo ya kuitwa “Most People Want This “
Akiongea kwenye mahojiano na Fredrick Bundala, Nahreel alidokeza kuwa hakutegemea Rick Ross angependa ngoma hiyo na kuongeza kuwa anaamini remix ya wimbo huo wa “Sip N Whine” itakuwa kubwa zaidi.
Kufikia sasa mtanzania pekee ambaye amefanya ngoma na Rick Ross ni Diamond Platnumz kupitia “Wakawaka” ngoma ambayo iliteka hisia za wengi pindi ilipotoka.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Joy Is Coming3:08
TUMWAMBIE MUNGU ASANTE0:49
Malaika2:49
NALOKINGA2:52
Stima - Buruklyn Boyz5:04
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Buwooma2:44
Alifata Hela3:53
Top stories
- Love
01 April
- My biography
02 April
- STREAM NEXARITO SONGS ON SPOTIFY
02 April
- Nobb challen
02 April


Leave your comment