Diamond Platnumz Adokeza Kuachia Ngoma Mpya Na Mabantu

[Picha: Instagram]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram

Msanii kutoka Tanzania Diamond Platnumz hivi karibuni amedokeza kuachia ngoma mpya na kundi linalofanya vizuri Tanzania kwa sasa, Mabantu.

Hivi karibuni Mabantu waliachia EP yao ya kuitwa “University EP” ambayo ina ngoma 8 huku ngoma yao ya kuitwa “Shemeji” waliyomshirikisha Baddest 47 ikiwa inafanya vizuri zaidi. Mabantu limeundwa na wasanii wawili ambao ni Twaah na Muuh

Kupitia ukurasa wa Instagram wa Mabantu, wasanii hao walichapisha video inayomuonesha Diamond Platnumz akiwa na Mabantu ambapo Platnumz alisifia EP mpya ya Mabantu ya kuitwa University EP na kuongeza kuwa Mabantu ni wasanii wenye vipaji kikubwa na tayari amefanya nao ngoma.

“Mabantu ni miongoni mwa vijana wenye talent sana nchini na tuna nyimbo mimi na wao na nimewashirikisha na nafikiri you can tell me kuwashirikisha wao inamaanisha hawa watu wabaya sana ni miongoni mwa ngoma ambazo zitatoka mwaka huu yaani Ramadhan ikishaisha yaani hapa hakalikki” alizungumza Diamond Platnumz.

Kando na Mabantu, collabo nyingine ambazo zinasubiriwa kutoka kwa Diamond Platnumz kwa mwaka huu ni pamoja na ngoma ambayo ameshirikiana na Marioo, Baba Levo pamoja na G Nako.

Leave your comment