Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Victoria Kimani Adokeza Collabo Mpya Na Wasanii Wa Tanzania
4 April 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Msanii wa muziki kutokea nchini Kenya Victoria Kimani hivi karibuni amedokeza kwamba Tayari ameshafanya collabo na wasanii wawili kutokea hapa nchini Tanzania.
Victoria Kimani ambaye mwaka 2021 alitetemesha Africa kupitia albamu yake ya “Spirit Animal” amedokeza kwamba kuna collabo inakuja kati yake na wasanii wawili wakubwa kutoka Tanzania. Victoria Kimani kwa sasa yuko nchini Tanzania kwa ajili ya mapumziko.
Akizungumza hivi karibuni kwenye kipindi cha The Switch, Victoria Kimani amedokeza kuwa ameshafanya collabo na wasanii wawili kutoka Bongo ambao hakuwataja na kuongeza kuwa kuna baada ya wasanii aliwaomba collabo lakini walikataa
“Kwa sasa nimeshafanya collabo na wasanii kutoka Tanzania. Nilishawahi kufanya hivyo pia zamani. Kuna baadhi niliwatafuta kwa ajili ya collabo lakini nadhani walijiona ni wakubwa sana. SiweI kuwataja” alidokeza Victoria Kimani
Ikumbukwe kuwa mwaka 2014 Victoria Kimani aliachia ngoma ya “Prokoto” ambayo aliwashirikisha Diamond Platnumz pamoja na Ommy Dimpoz.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- MOSS Kay
24 April


Leave your comment