Lyrics: Pita Huku - Dulla Makabila

 

[Picha: Instagram]

Pata na upakue Ubashiri wa Mechi mbalimbali ndani  ya Mdundo

We mama mtu mzima ndoa ingekupa heshima

Ila kutwa mitandaoni ulidate na vitoto

Unadai mmeo ana kitambi hawezi kupeleka moto

Aaah we mama pita huku

Uliaminiwa na kanisa ukaongoza kila misa

Ila ulijiona Mungu mtu kisa una pesa sana

Uliamini ushirikina na kula kondoo wa bwana

Mchungaji pita huku

Kutwa ulitukana hujachokozwa unagombana

Yani unalewa mpaka unajikojolea

Ila suala la sadaka ulikuwa unajitolea

We mlevi pita huku

Najua umekata tamaa ndo maana nakuona umeshika tama

 

Najua umekata tamaa ndo maana nakuona umeshika tama

Yani kazi yako Udj hilo halipingiki

Ila kila ulipofika muda wa ibada ulizima mziki

We DJ pita huku

We kwanza una laana chumbani kwako kuna mafuta kila kona

Unapenda kwa mpalange

Mtume hataki hata kukuona

Aaah we shoga pita huku

Unapenda kwa mpalange mtume hataki kukuona

Aaah we shoga pita huku

Nikikutazama unatia huruma maana naona hutoboi

Ushawatoa mina na zena na ulivyo fundi hukosei

Nawe dokta pita huku

Yani kufumba kufumbua ukajiona umefika

Sheria ukaipindisha masikini ukawakomesha

 

Na ukanenepa kwa rushwa

We hakimu pita huku

We mtoto wa kike ila nawe una demu

Na mademu wanakuita shemu

 

Aaaah inauma sana

Hata baba na mama hawataki hata kukuona

Maisha yako yote laana hauna mashine ila kazi tu kusagana

Tom Boy pita huku

Malaya unafanya mtu anatelekeza mpaka familia

Ada ya watoto wake ikifika kwako unakoga bia

Yani kudanga bongo huridhiki unaenda uturuki

Unakunywa vidonge hata mimba hushiki

Mbele ya shemeji zako unapita na kanga

Malaya ukiamua lako unampa mpaka mganga

We malaya pita huku

Mchawi unafanya watu wanafukuzwa kazi

Wengine unawauwa kwa kuwapa maradhi

Mchawi unawaachanisha mpaka wapenzi

Mchawi unawanyima watu usingizi

 

Mchawi oooh nakosa cha kuongea usiku unageuka paka mabati unarukia

Mchawi unaua mtu anaacha familia msibani unatokea unalia hadi unazimia

Mchawi ndo chanzo cha umasikini unapita kwenye pembe hivi milango huioni

Na uchawi mkaupeleka usafini Yani Lavalava hata aimbe vipi haonekani

We mchawi pita huku

https://www.youtube.com/watch?v=1aeVXLt5hOw

Leave your comment