Nkunku Na Majeraha Ya Goti Kuelekea Kombe La Dunia

[Picha:Instagram]

Mwandishi: Stellah Julius

Pata na upakue Ubashiri wa Mechi mbalimbali ndani  ya Mdundo

Habari za kusikitisha zimejiri katika timu ya Taifa ya Ufaransa mara baada ya Christopher Nkunku kupata majeraha ya goti wakati alipokuwa  akifanya mazoezi na timu hiyo.

Majeraha hayo ya goti yamejiri zikiwa zimebaki siku tano pekee kombe la dunia kuanza kutimua vumbi huko nchini Qatar.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 25 ambaye pia anakipiga huko RB Lepzig atakosa kushiriki kombe na dunia kutokana na majeraha hayo ikiwa hii ndiyo mara yake ya kwanza kushiriki kombe la dunia.

Ufaransa tayari wameshathibitisha majeraha hayo na pia inasemekana ya kuwa Randal Kolo Muani kutokea Einchracht Frankfurt ndiye ataichukua nafasi hiyo ya Nkunku.

Wakati hayo yanajiri Chelsea wanasemekana nao wanakamilisha mazungumzo ya kumsajili Nkunku katika msimu ujao na ya kuwa mazungumzo yako katika hali nzuri.

Leave your comment