Diamond ‘Gidi’, Zuchu ‘Mwambieni’ na Ngoma Zinazotamba YouTube Tanzania Wiki Hii

[Picha: YouTube]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Wiki ya kwanza kabisa ya mwezi Machi imewadia na bila shaka utakuwa na hamu ya kufahamu ni ngoma gani ambazo zinasikilizwa zaidi nchini Tanzania wiki hii kwenye mtandao wa YouTube. Makala hii imelenga kukupitisha kwenye ngoma tano ambazo zinafanya vizuri sana kwenye mtandao wa YouTube kwa wiki hii:

Pakua Nyimbo za Mac Voice Bila Malipo Kwenye Mdundo

Gidi - Diamond Platnumz

Diamond Platnumz amezidi kuonesha ubabe wake kwenye mtandao wa YouTube kwani ngoma yake ‘Gidi’ imezidi kufanya vizuri kwenye mtandao huo. Kufikia sasa ‘Gidi’ imeshatazamwa mara Milioni 3.6 kwenye mtandao huo ikiwa ndio inayoongoza kufanya vizuri zaidi kwa wiki hii.

https://www.youtube.com/watch?v=BRsoOKdmKic

Soma Pia: Diamond ft Wizkid, Anjella ft Ibraah na Collabo Zingine Bongo Zinazosubiriwa Sana na Mashabiki

Yanga Tamu - Marioo

Wale wapenzi wote wa mpira hasa timu ya Yanga bila shaka wameweza kurahani ngoma hii ya ‘Yanga Tamu’ ambayo ni kama remix ya ‘Bia Tamu’ kutoka kwa Marioo. Ikiwa zimepita siku 11 tu tangu kuachiwa kwake, ngoma hii ishatazamwa mara laki saba ishirini na nane kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=ERkUsjhXS_k

Omoyo Remix - Jane Miso & Harmonize

Ngoma ya ‘Omoyo Remix’ inazidi kuchanja mbuga kwenye mtandao wa YouTube. Hii pengine ni kutokana na mbinu nzuri za matangazo zilizotumika na Harmonize wakati anaachia ngoma pamoja na ubora wa kimashairi, mdundo na vionjo alivyotumia Harmonize na Jane Mix katika kibao hiki.

https://www.youtube.com/watch?v=Luj_vFdImVs

Pakua Nyimbo za Navy Kenzo Bila Malipo Kwenye Mdundo

Mwambieni - Zuchu

Kila shabiki wa muziki mzuri kutoka Tanzania tayari ameshasikiliza ngoma ya ‘Mwambieni’ pamoja na kuangalia video ya wimbo huo ambayo imejawa na uigizaji mzuri, uhalisia pamoja na vichekesho vitu ambavyo vimepelekea ngoma kubwa mno. Kufikia sasa, ‘Mwambieni’ imeshatazamwa mara Milioni 4.8 huko YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=j3kDvCgCG0Y

Toroka - Anjella ft Harmonize

Hii ni ngoma ambayo imemleta Anjella mpya ambaye anaonekana kufurahia maisha ya kustarehe na ‘kula bata’ hasa nyakati za usiku kwenye klabu na sehemu za starehe. Kufikia sasa, video ya ngoma hii imeshatazamwa mara Milioni 1.9 kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=M_8lSf5YUnE

Leave your comment