Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya: Bonge La Nyau Aachia EP Yake ‘Daktari Wa Mapenzi’
10 February 2022

[Picha: Nyimbo Mpya]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Rapa kutokea nchini Tanzania Bonge La Nyau ameachia EP yake mpya kabisa ya kuitwa ‘Daktari Wa Mapenzi’.
Kama jina linavyoashiria, ‘Daktari wa Mapenzi’ ni EP ambayo imesheheni jumla ya ngoma sita za moto ambazo zote zinagusia suala zima la mapenzi; kitu ambacho wengi wametafsiri kuwa ni katika kuadhimisha msimu huu wa Valentine.
Pakua Nyimbo za Kayumba Bila Malipo Kwenye Mdundo
Wasanii walioshirikishwa kwenye EP hii ni pamoja na Kayumba kwenye ‘Umenikosea’, Dayo ndani ya ‘Dam Dam’, Silvana kwenye ‘Nimechoka’ pamoja na Born Eyes kwenye ‘Waridi.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Rayvanny Aachia ‘Flowers II’ EP
Kikubwa kuhusu mradi huu ni kuwa Bonge la Nyau pamoj na ukubwa wake ameweza kufanya kazi na watayarishaji wa muziki wanaochipukia kama vile Dady Final, Bengs pamoja na Swabri Made It ambaye amehusika kutayarisha ‘Ndombolo’ ya kwao Kings' Music ambayo ni lebo ya Ali Kiba.
EP hii ni mradi wa kwanza wa Bonge La Nyau kwa mwaka huu wa 2022. EP hio inakuja baada ya miezi sita ya ukimya kutoka kwa msanii huyo ambaye mara yake ya mwisho kuachia ngoma ilikuwa ni Julai mwaka 2020 alipoachia ‘Madharau Part 1’ iliyofanya vizuri nchini.
Weekly Top 10 songs

omelette4:28
Kyuma Radio and weasel ft Spice Diana4:07
ONLY YOU JESUS5:44
Kupenda nishapenda zaani3:12
CHAMPION GAL3:00
Nigina2:27
KIDUCHU2:12
Wano Wano2:15
Zabike2:50
Melody Ft Tunche the best3:20
Top stories
- Get New Hit Songs From Mock
23 July
- Holy Boy (holyb374)
23 July
- PLS GUYS SUPPORT ME
24 July


Leave your comment