Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Hamisa Mobetto Adokeza Ujio wa Kolabo Zake na Otile Brown, Bien
18 January 2022

[Picha: Hamisa Mobetto]
Mwandishi: Brian Sikulu
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mwanamitindo Hamisa Mobetto, ambaye pia ni msanii kutoka Tanzania, amedokeza ujio wa kolabo baina yake na wasanii wakubwa wa Kenya. Hamisa Mobetto kwa sasa yupo nchini Kenya kwa shughuli ya kuchangisha pesa ya kusaidia watoto mayatima.
Kwenye kikao na wanahabari, Hamisa aliulizwa iwapo anapanga kufanya kazi na wasanii wa Kenya. Alisema kuwa tayari ako na kolabo na wasanii nyota Otile Brown pamoja na Bien kutoka Sauti Sol.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Rayvanny ft. Zuchu ‘I Miss You’ na Ngoma Zingine Mpya Zilizoachiwa Bongo Wiki Hii
Hii itakuwa mara ya kwanza Hamisa Mobetto kushirikiana na wasanii wa Kenya. Wasanii hao wawili waliotajwa, hata hivyo, si wageni kwenye tasnia ya muziki wa Tanzania, kwani wametoa kolabo na wasanii wa bongo.
Bien kupitia bendi la Sauti Sol amefanya kazi na Nandy, huku Otile Brown akiwa amefanya kazi na Alikiba pamoja na Harmonize. Kwa mujibu wa Hamisa, kolabo hizo zipo tayari na kilichosalia ni kuziachia tu.
"I have a song with Otile Brown, kolabo hizo zipo tayari na kilichosalia ni kuziachia tu. Tulishafanya iko tayari, tutatoa. I also have a song with Bien," Hamisa Mobetto alisema.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Tommy Flavour Aachia Ngoma Mbili Mpya ‘Lay Down’ na ‘Kidogo’
Msanii huyo hata hivyo hakutoa tarehe kamili ambazo nyimbo hizo zitatoka au maudhui yake. Kolabo hizo zinatarajiwa kumpandisha Hamisa Mobetto cheo kwenye tasnia ya muziki na kumpa mashabiki hata zaidi kutoka Kenya.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April


Leave your comment