Nyimbo Mpya: Ngoma Tano Mpya Zilizoachiwa Bongo Wiki Hii

[Picha: The Citizen]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Soko la muziki nchini Tanzania limeendelea kukua kwani wasanii wameendelea kutoa kazi kila kukicha na wiki hii mambo hayajakuwa tofauti sana kwani wasanii Hamisa Mobeto, Aslay, Bright Music, Killy na wengineo wameendelea kuendeleza utaratibu huo.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Hamisa Mobetto Aachia Wimbo Mpya ‘Ex Wangu’ [Video]

Zifuatazo ni ngoma tano kali zilizotoka wiki hii:

Mwisho – Killy

Wimbo wa pili kutokea kwa Killy tangu alipotia wino kwenye label ya Konde Gang. Bila shaka, Killy ameendelea kuonesha kuwa yeye bado ni fundi wa kuandika nyimbo za mapenzi. kufikia sasa, wimbo huu umetazamwa mara milioni moja nukta saba kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=1jag9EhRvkk

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Lulu Diva, Lava lava Waachia Wimbo Mpya ‘Samahani’ [Video]

Shangingi Mtoto - Aslay

Baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kutoa wimbo, Aslay anarudi kwa kishindo na wimbo wake wa ‘Shangingi Mtoto’. Kwenye wimbo huu, Aslay ambaye ni maarufu kwa uandishi wa nyimbo za mapenzi humu anaelezea jinsi watu wanavyofanya maamuzi hasi maishani hivyo kuwagharimu.

https://www.youtube.com/watch?v=xu1xSh63WqE

Demu Wangu - Bright ft Meja Kunta

Muziki wa Singeli umeendelea kushika kasi nchini Tanzania kwani msanii Bright nae ameamua kushirikiana na Meja Kunta kwenye wimbo huu ambao umetoka siku sita nyuma. 

https://www.youtube.com/watch?v=wx0hcK82IV4

Ex Wangu Remix - Hamissa Mobeto ft Seneta Kilata

Mwanamuziki Hamissa mobetto ameendelea kuonesha kuwa muziki hauna mipaka baada ya yeye kuamua kufanya muziki aina ya singeli. Akishirikiana na Seneta Kilata, Mobetto ameonesha umaridadi mkubwa kwenye wimbo huu ambao mpaka sasa video yake imetazamwa mara milioni moja kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=CmSgffQYaSo

Imoo - Frida Amani ft Mimi Mars

Ni muziki mzuri tu unatokea pale ambapo wasanii wawili wakike wanapoamua kushirikiana kutengeneza wimbo. ‘Imoo’  ni wimbo wenye miondoko ya Hip-hop na mdundo wa kuchezeka na kama kawaida Frida Amani amechana huku Mimi Mars akifanya kiitikio cha wimbo huu. Wimbo huu hauna video rasmi bado lakini inategemewa itaachiwa hivi karibuni.

https://www.youtube.com/watch?v=PkzUs4kvWck

Leave your comment