Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Kimambo Beats Ajibu Madai Kuwa Midundo Zake Zinafanana
11 June 2021

[Picha: Kimambo Touches Facebook]
Mwandishi: Brian Sikulu
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania Kimambo Beats amejitokeza kujibu madai kwamba midundo zake zinafanana kila wakati. Akizungumza wakati wa mahojiano ya hivi karibuni, Kimambo Beats alipuuzilia mbali ripoti hizo akisema kuwa hazina msingi.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Aslay Aachia Wimbo Mpya 'Vumilia'
Aliongeza zaidi kuwa watu wanaotoa madai hayo hawaelewi kazi yake vizuri. Kulingana na Kimambo, hajawahi kurudia midundo yake na hubadilika kila wakati akifanya kazi na wanamuziki tofauti.
Alitoa mfano wa wanamuziki ambao amefanya nao kazi na jinsi midundo ilikuwa tofauti na kila mmoja.
Miongoni mwa wanamuziki bora ambao mtayarishaji wa muziki huyo amefanya kazi nao ni Nandy, Jux, S2kizy, Shetta kati ya wengine.
Soma Pia: Aslay vs Marioo: Nani Bora Zaidi katika mziki wa RnB?
Kimambo Beats, hata hivyo, alifafanua kwamba baadhi ya mashabiki wake wanaweza kukosea na mradi ambao aliulifanya zamani. Katika mradi huo, Kimambo Beats alitengeneza mdundo mmoja na kuwapa wasanii tofauti kuimba wakitumia.
"Audience mashaidi, toka nipige Papa ya Gigy Money sijawahi kurudia. Toka nipige banana ya Dogo Janja sijawahi kurudia. Toka nipige nyimbo zangu zote almost ambazo zimefanya vizuri sijawahi kurudia style," Kimambo alisema.
Kimambo pia alifunua kuwa hivi karibuni atazindua mradi wa muziki ambao amekuwa akiufanyia kazi kwa muda mrefu sana.
Weekly Top 10 songs

KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
CHAMPION GAL3:00
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- NEW SONG ALERT
16 May
- Generation
16 May
- Boom Shakatah means
17 May
- Date of birth
15 May


Leave your comment