Nyimbo Mpya Zilizoachiwa na Zuchu, Rayvanny, Mbosso na Lava Lava Mwezi Mei 2021 [Video]

[Picha: Rayvanny Instagram]

Mwandishi: Omondi Otieno

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Kelebe - Rayvanny ft Innoss’B

Huu ndio wimbo ulioachiwa na Rayvanny akimshirikisha msanii gwiji kutoka Congo Innoss’B. Mwezi Mei ‘Kelebe’ ilichukua nafasi ya kwanza kwenye trends na watazamaji zaidi ya milioni tatu nukta mbili kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=V7sBxHz_nHE

Soma Pia: Diamond Platnumz Ateuliwa kwa Tuzo za BET 2021

Yes - Mbosso ft Spice Diana

Huu ni wimbo wa kumuomba mchumba kuwa mke wa mtu au tuseme harusi. Kwenye huu, wimbo Mbosso alimshirikisha Spice Diana kutoka Uganda. ‘Yes’ ni mojawapo ya ngoma kwenye ‘Definiion of Love’ album alioachia Mbosso.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Ngoma 5 Kali Zilizoachiwa na Wasanii wa Konde Gang Mei 2021[Video]

https://www.youtube.com/watch?v=NClIIN8FgF4

Komesha – Lava lava

‘Komesha’ ni wimbo mpya kutoka kwa msanii Lava Lava. Katika ngoma hii, Lava Lava anapigania penzi lake. Kufikia sasa, ‘Komesha’  ina watazamaji zaidi ya milioni moja.

https://www.youtube.com/watch?v=XmT_CsFAtqc

Sere- Olakira ft Zuchu

Kwenye wimbo huu, msanii wa Nigeria Olakira amemshirikisha Zuchu. Hii majowapo ya ngoma kutoka kwenye ‘4Play’ EP yake Olakira. Kwa sasa ngoma hii ina watazamaji zaki ya milioni moja nukta tisa kwenye YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=wht8D5mekJ8

Kazi Iendele – Zuchu na Rayvanny

Zuchu na Rayvanny waliachia nyimbo mbili tofauti zenye mada sawa ‘Kazi Iendelee’.

Wawili hawa waliachia kazi hii kumsifia rais wa Muungano wa Tanzania Bi. Samia Suluhu.

Katika wimbo wa Zuchu, anahadithia historia ya Rais Suluhu katika siasa kuanzia alipokuwa makamu wa Rais chini ya uongozi wa aliyekuwa rais wa Tanzania marehemu Dkt. John Pombe Magufuli alieaga mwezi mmoja uliopita.

https://www.youtube.com/watch?v=DVI01LmfY0I

Kwa upande wake Rayvanny alimsifia Rais Samia kama mama wa taifa na kama wananchi wanampa pongezi kwa kuhimiza kuwa 'Kazi iendelee'.

Katika mistari yake, anaanza kwa kukumbuku za kifo cha marehemu rais Magufuli jinsi wanachi walivyohuzunika na kuvunjika mioyo kuhusu kifo cha rais huyo.

Rayvanny anaimba kuwa 'Kazi iendelee' katika sekta mbali mbali kwani aliye kwenye usukani anajali maslahi ya wananchi wake.

https://www.youtube.com/watch?v=rj3jXerJ1kA

Leave your comment