Pakua Mixtapes Tano Kali za Hip Hop Kutoka Bongo kwenye Mdundo

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Fani ya muziki wa hip hop  nchini Tanzania imekuwa ikibadilika kwa miaka mingi. Awali muziki wa hip hop wa Tanzania ulikuwa ndio  Bongo Flava asili.

Waliotambulika katika mziki hii walikua TMK Wanaume original, Dog Malik, JCB, Watengwa,Chindo aka Umbwax, Donii, Wadudu wa dampo, Jambo Squad, Gnako, Weusi, na wengineo.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Mbosso, Anjella Wang'aa Kwenye Nyimbo Tano Bora Wiki Hii

Rapa wa Tanzania waliangazia kile walichokiona karibu yao. Maudhui yao nyimbo  yakiwa juu ya umasikini, hatari za HIV, rushwa na ugumu wa jumla wa kukulia katika taifa linaloendelea wakati ule.

Huku tukijaribu kuangazia ukuaji wa mziki huu wa hip hop tunakupa fursa ya kupakua mixtape Tano Kali kutoka Bongo.

Mr Blue, Nandy, Khaligraph, Masauti, Wakadinali, Darassa, latest Bongo HipHop

Huu ni mchanganyiko wa nyimbo kali kutoka kwa wasanii tajika kutoka Kenya na Tanzania.Hizi ni nyimbo za maudhui ya mapenzi na mdundo wake ni wakuburudisha. Wasanii husika katika nyimbo hizi ni kama vile Nameless, Khaligraph,Masauti, Darassa, Wakadanili miongoni mwa wengineo.Pakua mixtape hii ufurahie na umpendaye.

TMK Wanaume, Chege, Professor Jay, Gadafy, Nonini, QTAC, Ousmane, Amani - BONGO 

Kwenye mix hii ya DJ Bee inayoleta pamoja wasanii kadhaa wa hip hop asili kama vile Proffessor Jay, Gaddafi, TMK Wanaume, Chege, Ousmane miongoni mwa wengine zaidi.Pakua mixtape hii utambue ufundi wa mziki wa hip hop asili ya Kiswahili.

Bamboo, Chege, TMK Wanaume, Collo, Temba

Katika kufaruhia mziki wa hip hop barani Afrika mashariki Tmk wanaume, Mwana Fa, Ay ni miongoni mwa wasanii tajika kutoka Tanzania walioupa mziki wa hip hop fursa ya kukubalika. Hivyo kwenye mixtape hii DJ Bee anakupa mchanganyiko wa nyimbo kutoka kwa baadhi ya wasanii hao tajika katika fani ya mziki wa hip hop.

Rosa Ree, Roberto, Darassa, Nameless, Sho Madjozi,

Hii ni mix inayoonyesha ubabe wa Rosa Ree kwenye mziki wa Hip hop na kuongeza mdundo wa nyimbo za Darassa. Hivyo jumla katika mixtape hii ya DJ Bee ni kuonyesha uzito wa wanamziki kama Nameless, Sho Madjozi na wengine wengi.

 

Leave your comment