Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
"Hii Ndio Nyimbo Yangu Ninayoiheshimu”- Aslay
31 July 2018

Aslay Isihaka ameanza muziki akiwa mdogo na amefunguka kuwa katika ngoma zake ambazo amewahi fanya hadi sasa wimbo anaouheshimu ni 'Naenda kusema kwa mama'.
Aslay amesema hayo kwenye KIKAANGONI ya East Africa Television, inayoruka kila Jumatano kupitia ukurasa wake wa Facebook na kutoa sababu za kuuheshimu wimbo huo kuwa, ndiyo wa kwanza mara baada ya kusainiwa kama msanii.
“Katika ngoma zangu, wimbo ninaouheshimu ni 'Naenda kusema kwa mama' maana ndiyo kwanza nilikuwa nimesainiwa kama msanii chini ya Mkubwa na Wanawe, hivyo wimbo huo ndio umenipa heshima hadi leo maana ulifanya nipokelewe vizuri na mashabiki wa muziki nchini”, amesema Aslay.
Msanii Aslay alianza kufahamika mwaka 2011 baada ya kutoa wimbo wake wa kwanza wa ‘Naenda kusema kwa mama’ na baadaye alitoa nyimbo nyingi peke yake kabla ya kuingia katika kundi lililokuwa na wasanii wanne likiitwa 'Yamoto Band' ambalo limevunjika na mpaka sasa anaendelea kufanya vizuri akiwa peke yake.
Source: eatv.tv
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April


Leave your comment