Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Barnaba Aifungia Kazi Albamu Yake
28 June 2018

Msanii wa Bongo Flava, Barnaba ameweka wazi kuwa amekamilisha albamu yake ambayo inatarajiwa kutoka mwezi ujao.
Albamu ya muimbaji huyo ambayo inakwenda kwa jina la Gold itakuwa na nyimbo zipatazo 18. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ndipo ameeleza kukamilika kwa albamu hiyo.
“Narudia tena kusema hii ni Gold na mgodi umebeba dhaabu ambazo zimepikwa muda mrefu sana, sitaki kusema mengi I can’t wait kwa kweli,” amesema Barnaba.
Awali albamu hiyo ilipangwa kutoka February 2018 lakini ikahairishwa hadi July 2018 kutokana na kile Barnaba alichoeleza kuwa wadhamini wake wakuu watatu walipendelea hivyo.
Mwanzoni mwa mwaka huu katika kipindi cha The Playlist, Times Fm, Barnaba alisema albamu hiyo itakutanisha wasanii wengine kutoka Kenya Uganda na Nigeria.
Wasanii waliotajwa kuwepo katika albamu hiyo ni pamoja na Juliana Kanyomozi na Jose Chameleon kutoka Uganda. Kutoka Bongo kuna Vanessa Mdee, G Nako, Ben Pol, Aslay, Barakah The Prince, Linex na Joh Makini.
Source: bongo5.com
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April


Leave your comment