Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Jide Awafariji Vijana
28 March 2018

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ni mkongwe kwenye game na aneendelea kukimbiza, Judith Wambura au Jaydee, ametoa sababu ya kuandika wimbo wake mpya wa 'Anaweza' ambao amemshirikisha msanii wa Jamaica Luciano.
Akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television, Jaydee amesema vijana wengi sasa hivi wamekata tamaa na maisha kutokana na mambo mbali mbali yanayowakabili, hivyo akaona ni vyema iwapo atatunga kitu cha kuweza kuwafariji.
“Vijana wengi sana kwa kipindi hiki wameonakana kukata taa, na kuna vitu vingi ambavyo wanapitia, mambo mengi yamekuwa kelee, party, fake life, nimefikiri ni muda muafaka kuwapa moyo watu ambao wamekata tamaa kuwaambia kuwa wanaweza”, amesema Lady Jaydee.
Kazi hiyo mpya ya Jaydee audio imetengenzwa na mpenzi wake Spice huku video ikitengenzwa na Justine Campos wa Afrika Kusini.
Courtesy: eatv.tv
Weekly Top 10 songs
Top stories
- The Marathon
25 April
- MOSS Kay
24 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- Naphlic_fx
24 April




Leave your comment