TANZANIA: Diamond Athibitisha Kolabo ya Harmonize na Staa Mkubwa Marekani

Bosi wa WCB, Diamond Platnumz amemwaga mchele hadharani – Ameweka wazi kuwa Harmonize ana kolabo na staa mkubwa kutoka nchini Marekani.

Akiongea na Dizzim Online, Diamond amethibitisha kuwa kuna kolabo ya Harmo ambayo amefanya na rapper Tyga.

“Harmonize kuna nyimbo kafanya na wasanii wa ndani na nje. Harmonize ana nyimbo mpaka na Tyga, ana nyimbo Harmonize na Tyga amefanya,” amesema Diamond.

Diamond ameongeza kuwa yeye sio mbinafsi kwani hata albamu yake ameahirisha mara mbili kuitoa ili Lava Lava na Mbosso waachie ngoma zao.

 

Source: bongo5.com

Leave your comment