Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Ukiwa Msanii Ni Lazima Uwe Na Thamani Yako Ili Kuogopeka – Country Boy
6 March 2018

Msanii wa muziki Bongo, Country Boy amesema msanii ni lazima ajitengezee mazingira ya upekee kwa sababu hiyo ndio biashara yake.
Rapper huyo amesema kitu hicho kimemfanya baadhi ya wasanii kuogopa kufanya naye ngoma kutokana na kiwango ambacho amekiweka katika muziki wake.
“Ukiwa msanii ni lazima uwe na value yako, usiwe tu wa kawaida, hiyo ndio biashara siku zote. Navyojiweka na mazingira ambayo nimetengeneza ni mazuri na kunifanya niweze kuogopeka hata ukija unakuja na kazi bora,” Country Boy ameiambia Bongo5.
“Hata muziki wangu nauchukulia serious zaidi, kila ninachokifanya lazima ni kiogope na nikiheshimu, sijichukulii poa,” amesisitiza.
Country Boy kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Mwaaa’ aliyoshirikiana na Moni ambapo kwa pamoja wanaunda kundi la MoCo.
Source: bongo5.com
Weekly Top 10 songs
Top stories
- The Marathon
25 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- Naphlic_fx
24 April
- TRUE LOVE
26 April




Leave your comment