KENYA: Bahati na Mkewe Diana Marua Wapata Mtoto Wao wa Kwanza

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Bahati amethibitisha kupata mtoto wake wa pili wa kike.

Bahati amepata mtoto huyo na kupitia kwa mkewe Diana Marua ambaye amejifungua mapema Jumatano hii. Muimbaji huyo ameonyesha furaha yake kupitia mtandao wa Instagram na kutaja jina la mtoto wao huyo kuwa ni Heaven.

“GLORY TO JESUS!!! This Morning this Girl @Diana_Marua has given me the greatest gift of Life #BouncingBabyGirl 3.24kgs. Help Us Welcome @HEAVENBAHATI,” ameandika Bahati.

Mtoto huyo anakuwa wa pili kwa Bahati, baada ya wa kwanza aliyezaa na ex wake, Yvette Obura.

Source: bongo5.com

Leave your comment