Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Alikiba Aeleza Umuhimu wa Elimu kwa Msanii, ‘Achana na Wanaoimba Ujinga’
19 October 2017

Hitmaker wa ngoma Seduce Me Alikiba amezungumzia umuhimu wa msanii kuwa na elimu.
“Unajua ubongo wako ukiwa active utaweza kufikiria vitu vya msingi zaidi, achana na watu wanaoimba ujinga, ni kwa sababu tu ya talent lakini elimu ni ya muhimu sana kwenye kila kitu,” amesema Alikiba.
Katika mahojiano na Bongo5 ameeleza kuwa msanii akiwa na elimu kutamfanya kuweza kufikiri kwa undani zaidi na kumfanya yule anayemsikiliza kutambua msanii husika ni wa namna gani.
“Ukiwa na elimu kama wewe ni msanii ni rahisi kuonyesha watu ubongo wako ukoje, kwa sababu mkasa na visa vipo na maneno yapo lakini utamfanya mtu afikirie huyu alifikiria nini” amesema.
Alikiba bado anafanya vizuri na ngoma Seduce Me ambayo hadi kufikia sasa inaviews milioni 6.9 katika mtandao wa YouTube na ahadi yake ni kuwa ikifikisha views milioni 10 atatoa ngoma mpya.
Source: bongo5.com
Weekly Top 10 songs

KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
CHAMPION GAL3:00
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- NEW SONG ALERT
16 May
- Generation
16 May
- Boom Shakatah means
17 May
- Date of birth
15 May


Leave your comment