TANZANIA: Nataka kusimama mimi pamoja na mashabiki zangu - Ruby

 

 

 

 

Msanii wa Bongo Fleva, mwanadada Ruby ambaye amewahi kutamba na wimbo wake wa "Na Yule' amefunguka na kusema kwa sasa amebadili uongozi wake na kujisimamia yeye kwani anataka kusimama yeye pamoja na mashabiki zake.

Ruby alisema hayo kwenye kipindi cha eNewz na kudai kuwa yeye aliamua kubadili uongozi kwa sababu anataka kusimama yeye kama yeye kwenye muziki kwa kutegemea mashabiki wake, pia Ruby anadai Tanzania ukimchana mtu ukweli unaonekana wewe ni mkorofi au mgomvi.

"Unajua hata mtoto anapokuwa kwa wazazi inafika wakati anahitaji kuanza maisha yake mwenyewe, hivyo mtoto akiondoka kwa wazazi haina maana kuwa hauna wazazi 'No' wala haina maana kuwa umeondoka nyumbani kuna matatizo bali unakuwa umeanza maisha yako mwenyewe, ni sawa na mimi saizi nimebadili uongozi wangu na niko mimi kama mimi kwani nataka kusimama pamoja na mashabiki zangu. Watu wanasema sijui mimi ni mkorofi hao ni wao kwani mtu ukimchana ukweli unaonekana wewe ni mkorofi ni bora ukamwambia mtu ukweli kwani ukweli utakuweka huru" alisema Ruby

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

Leave your comment