Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
EXCLUSIVE (TANZANIA) – Ngoma mpya ya Temba yachelewa kutoka, Jua ni sababu gani na nani kasababisha!
30 December 2015

Msanii Temba amedai kuwa Hanscana ndiye amesababisha kuharibika kwa ratiba yake ya kuachia video ya wimbo wake mpya, Fundi.
Rapper huyo ambaye miezi michache iliyopita aliwaahidi mashabiki wake kuachia wimbo wa ‘Fundi’ aliowashirikisha Yamoto Band na Jokate, na kusema kuwa kazi hiyo haitoweza tena kutoka mwaka huu.
“Nimeshindwa kutoa ngoma kwasababu nilipanga kutoa audio na video lakini director Hanscana akawa amesafiri South Africa kwa short project, lakini akakaa mwezi mmoja na nusu ndio maana nikashindwa kutoa project kwa nilihitaji kutoa video na audio” alisema Temba.
Pia Rapper huyo ametoa sababu nyingine ni kuingiliana na ratiba kati yake na Chege. Ambapo wasanii wote hao wapo chini ya management moja ya Mkubwa Fella.
“Kitu kingine wakati Chege anaenda Afrika Kusini na mimi nilitakiwa kwenda lakini nilishindwa kutokana na passport yangu iliisha muda. So nikaona bora nisupport kazi ya Chege halafu mwakani yakwangu ndio itoke”.
Source: Bongo5
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- Grateful
25 May


Leave your comment