Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
EXCLUSIVE (TANZANIA) – Kuweza kutoka ubunifu unahitajika kwa muziki wa sasa– Cyril
18 December 2015

Rapper Cyril Kamikaze, amesema muziki wa sasa sio tu kufanya video na ngoma kali ili uweze kutoka bali unahitaji kutumia ubunifu zaidi kukidhi viwango vyenye ubora na kufikia soko la kimataifa.
Mwanamuziki huyo amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio kuwa watu wengi wanafikiri ukiwa na video nzuri ndio unafanikiwa.
“Unaweza ukawa na video kali halafu usihit, muziki ni zaidi ya chupa kali, ukirudishwa miaka fulani nyuma ngoma kali ndio ilikuwa inahit, lakini sasa msanii kupigwa na redio atataka kitu fulani. Hivyo muziki ni zaidi ya ngoma kali, zaidi ya chupa kali”, alisema Kamikaze.
Msanii huyo ameachia wimbo pamoja na video yake siku chache zilizopita ‘Shori’, pia amesema tayari ana album mbili ambazo zitatoka mwakani bila kujali kama zitamlipa au la.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- Grateful
25 May


Leave your comment