Rasmi, Jay Melody Aachia Albamu Yake Ya Kwanza Ya Kuitwa "Therapy"

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga

Baada ya kuidokeza kwa muda mrefu, hatimaye Jay Melody ameachia albamu yake ya kwanza ya kuitwa "Therapy"

"Therapy" ni albamu iliyoshehheni ngoma 12 ambapo kati ya hizo ni ngoma mbili tu ambazo Jay Melody ameshirikisha wasanii wengine, Phina akiwa mmoja wao.

Kwenye albamu yake ya "Therapy" Jay Melody kwa kiasi kikubwa ameimba kuhusu mapenzi. Kupitia ngoma kama "Nahodha" "Wa Peke Yangu" na nyinginezo Jay Melody anafurahi na kusimulia hadithi nzuri za mapenzi.

"Therapy" ni albamu ya kwanza kwa Jay Melody tangu aanze muziki na inatarajiwa kufanya vizuri ndani na nje ya Tanzania

Leave your comment