Mocco Genius Akutana Tena Na Ali Kiba Kwenye "Mchuchu"

Image Source: Online

Writer: Charles Maganga 

Kama uliipenda combo ya Mocco Genius na Ali Kiba basi habari njema ni kwamba wasanii hao wawili wamerudi tena na ngoma nyingine ya kuitwa "Mchuchu"

Kabla ya ngoma hii Mocco Genius na Ali Kiba walikutana kwenye "Napendwa II" ngoma ambayo iliingia sokoni Agosti ya mwaka 2022.

Kwenye "Mchuchu" Mocco Genius na Ali Kiba wanatumia vionjo vya Bongo Fleva kumsifia na kutoa heko kwa binti ambaye wako naye kwenye mahusiano.

"Mchuchu" ni ngoma ya pili kutoka kwa Mocco Genius kwa mwaka huu na inatarajiwa kufanya vizuri ndani na nje ya Tanzania

https://youtu.be/Dbrcsw_lrCM?si=WkDHiRuBaEfge5Ms

Leave your comment