Stamina Afichua Marapa Wawili Kutoka Kenya Aliowashirikisha Kwenye Albamu Yake Inayotarajiwa Kuachiwa Hivi Karibuni

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Wakati wapenzi wa muziki Tanzania wakisubiri kwa hamu albamu ya rapa Stamina, msanii huyo hivi karibuni amewataja wasanii wawili kutoka Kenya watakaoshiriki kwenye albamu hiyo. 

Akiwa kwenye mahojiano hivi karibuni, Stamina alidokeza kuwa King Kaka na Meja watakuwepo kwenye albamu yake ambayo inatarajiwa kuingia sokoni hivi karibuni 

"Wapo wengi sana. Wapo kina Meja Kenya, King Kaka na wengine sikutajii kwa sababu kuna wengine kutoka Rwanda. Kuna Ufaransa. Nna watu wengi" alizungumza Stamina.

Kufikia sasa bado Stamina hajaweka wazi jina la albamu hiyo, jumla ya ngoma zitakazokuwepo au hata tarehe ambayo albamu hiyo litaingia sokoni.

Leave your comment